Home » 2016 » June » 18


Kampuni ya Microsoft imekuwa ya hivi karibuni kujiunga na biashara ya kuuza bangi katika majimbo ya nchini Marekani ambako inaruhusiwa kwa mujibu wa sheria za majimbo hayo.
Kampuni hiyo imeungana na kampuni nyingine "Kind Financial - inayotengeneza programu za kusaidia wadhibiti kufuatilia uzalishaji na mauzo ya bangi.
Majimbo kadhaa nchini Marekani yameruhusu uuzaji wa bangi kwa matumizi ya kimatibabu na kujistarehesha, japo imeharamishwa chini ya sheria kuu za nchi hiyo.
Category: HABARI | Views: 366 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)




Magazeti leo juni 18 jumamosi na habari kwenye kurasa za mbele na nyuma haya hapa
Category: MAGAZETI | Views: 341 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)


Timu ya taifa ya Italia imefika hatua ya muondoano katika michuano ya ubingwa wa Ulaya baada ya kujipatia ushindi dhidi ya Sweden.

Ushindi wa Italia ulitokana na bao la pekee la mechi hiyo, lililofungwa na Eder dakika za mwishomwisho.

Ishara zilionesha kana kwamba mechi hiyo ingemalizika sare tasa hadi pale Eder alipokimbia na kufikia mpira kutoka kwa Simone Zaza nje kidogo ya eneo la hatari dakika ya 88.
 
Category: HABARI | Views: 287 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)



Mzambia Obey Chirwa rasmi amesaini kuichezea Yanga, ameingia nayo mkataba wa miaka miwili na kufunga idadi ya wachezaji saba wa kulipwa.

Chirwa anayetokea FC Platinums ya Zimbabwe amesaini mkataba huo leo mbele ya Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deudetis.

 
Category: MICHEZO | Views: 320 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)




WAZIRI wa Nchi katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kushirikiana na viongozi wa Mkoa kuhakikisha kuanzia leo hakuna mfanyabiashara atakayefanya biashara katika maeneo ya ‘mataa’
Category: HABARI | Views: 304 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)



IDARA ya Uhamiaji iko katika mchakato wa kuanzisha mahakama ya kijeshi ili kuwaadhibu maofisa wake wanaokiuka taratibu kama ilivyo kwa majeshi mengine nchini.

Hayo yalisemwa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Yusufu Masauni, wakati akijibu maswali mbalimbali ya wabunge.
Category: HABARI | Views: 335 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)



NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jaffo, amewataka wabunge kuacha kuwapelekea viongozi ‘vimemo’ vya kuwaombea msamaha watumishi wasio na maadili wa hospitali mbalimbali nchini watakapokuwa wanatumbuliwa.
Category: HABARI | Views: 316 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)



TAMASHA la Kigoda cha Mwalimu Nyerere, linaloandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, limetoa tuzo ya pekee kwa mwanzilishi wa Vikundi vya Benki za Kijamii (Vicoba), anayejulikana kwa jina la George Swevetta kwa mchango wake wa kukuza na kuimarisha uchumi kwa watu nchini.
Category: HABARI | Views: 354 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)



MTOTO mwenye ulemavu wa ngozi (albino) mwenye umri wa miaka mitatu, mkazi wa wilaya ya Itilima, mkoani Simiyu hivi karibuni amenusurika kuuawa kwa kukatwa mapanga, baada ya bibi yake kudaiwa kumuuza kwa wauaji hao ili waweze kuchukua sehemu ya viungo vyake.
Category: HABARI | Views: 303 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)

Akizungumza baada ya mtendaji huyo kuhamishwa, mmoja wa wakazi hao,  Ernest Bunyutule amesema jana kuwa: “Mtendaji huyu ameonyesha uwezo mkubwa kwa kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kutatua kero za wananchi. Hatupo tayari kumpokea mtendaji mwingine.”
Category: HABARI | Views: 286 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)




Hamis amemweleza Jaji mkuu kuwa yupo hatarini kupoteza haki yake ya urithi aliyoipigania tangu 2006 baada ya baba yake, Mohamed Hamis kufariki dunia.

Dar er Salaam. Kijana Abdullatif Hamisi (23), amemwandikia barua Jaji Mkuu akilalamikia hatua ya Mahakama Kuu kutoa hukumu mbili tofauti na kumnyima haki ya kupata mgawo wa urithi wa mali ya baba yake.
Category: HABARI | Views: 321 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-18 | Comments (0)