Urusi inasema kuwa Rais Erdogan wa Uturuki ameomba msamaha kwa hatua ya taifa lake, kuidungua ndege ya kivita ya Urusi karibu na mpaka na Syria mwaka jana.
Katika ujumbe ulioandikwa ndani ya barua hadi Kremlin kwa Rais Putin, Bwana Erdogan alielezea masikitiko yake makubwa kwa kile kilichofanyika, huku akisema anataka kurejesha uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili.