Home » HABARI
« 1 2 ... 20 21 22 23 24 ... 32 33 »
Jaji nchini Uganda ametoa amri kuwa kesi ya kiongozi wa upinzani nchini humo Kizza Besigye, ifanyike mahakamani kwa makosa ya uhaini na wala sio kwenye gereza lenye ulinzi mkali ambapo anazuiliwa.
Category: HABARI | Views: 272 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-15 | Comments (0)



Roboti kwa jina Pepper, iliyotengenezwa kuelewa hisia za watu inatarajiwa kuanza kazi mpya kama karani wa mapokezi katika hospitali mbili nchini Ubelgiji.

Roboti hiyo itakuwa ya kwanza kuhudumu katika jumba la matibabu baada ya roboti nyengine kuwekwa katika maduka ya uuzaji bidhaa, benki na vituo vya treni.

Hospitali moja inamipango ya kuajiri roboti zaidi kwa miaka 10 ijayo.

Baadhi ya wataalamu wamehoji umuhimu wa roboti za kijamii kama vile Pepper.
Category: HABARI | Views: 292 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-15 | Comments (0)



WAKATI kesho Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikitarajiwa kutimiza azma yake ya kuzima simu ‘feki’ za mkononi, upo mtikisiko na kizaazaa miongoni mwa watumiaji wa vifaa hivyo vya mawasiliano, wakisaka mbadala na wengine wakisubiri kuona kama ‘yatatimia’.
Category: HABARI | Views: 298 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-15 | Comments (0)



MWANASIASA mkongwe nchini na Naibu Waziri Mkuu mstaafu, Agustine Mrema amewataka wapinzani kumwacha Rais Dk. John Magufuli afanye kazi yake kwa kuwa amechaguliwa kihalali na bado hajamaliza hata kipindi cha kwanza cha uongozi wake.
Amewatahadharisha wananchi kuwa makini na wanasiasa kwa kuwa wapo baadhi wasio na nia njema na nchi badala yake wamekuwa wakipigania maslahi yao binafsi hata kama nchi inaweza kuingia kwenye majanga.
Category: HABARI | Views: 291 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-15 | Comments (0)



Chadema imeondoa mahakamani kesi dhidi ya polisi ya kupinga amri ya kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara, baada ya kubainika mapungufu ya kisheria katika hati yao ya mashtaka. 
Akizungumza na mwandishi wa habari hii ofisini kwake jana, Jaji Mohamed Gwae aliyepangwa kusikiliza shauri hilo alitaja mapungufu ya kisheria yaliyobainika kwenye hati ya mashtaka ya Chadema kuwa ni pamoja na kumjumuisha katika hati ya mashtaka Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Nsato Mssanzya, ambaye kisheria alistahili kufunguliwa shtaka katika masjala kuu (main registry). 
Category: HABARI | Views: 267 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-15 | Comments (0)



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh, Mwigulu Nchemba(kulia), na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira(kushoto) wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni, muda mfupi baada ya Rais Dkt. John Magufuli kumwapisha Waziri Mwigulu Nchemba kuongoza wizara hiyo leo.
Category: HABARI | Views: 316 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-13 | Comments (0)

Eritrea imeishtumu Ethiopia kwa kutekeleza shambulio katika mpaka wake ambao una ulinzi mkali.

Wakazi katika eneo la Tsorona wanasema wamesikia milio ya risasi na kuona wanajeshi wakielekea katika mpaka.

Hata hivyo Waziri wa habari wa Ethiopia amesema hafahamu lolote kuhusu vita hivyo.

Zaidi ya watu laki moja walifariki katika mapigano yaliyodumu mika miwili na nusu katika ya mataifa yote mawili.

Category: HABARI | Views: 306 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-13 | Comments (0)

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha mawaziri wapya wa mambo ya ndani na yule wa kilimo siku mbili tu baada ya kutangaza mabadiliko madogo katika baraza lake la mawaziri.

Jumamosi iliyopita rais Magufuli alitangaza uteuzi wa mbunge wa Buchosha Dkt. Charles John Tizeba kuwa waziri wa kilimo, mifugo na uvuvi.

Category: HABARI | Views: 293 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-13 | Comments (0)

Marafiki wawili na wafanyabiashara nchini Uganda Mr Steven Wesonga na Mr David Woisi wamekubaliana wikend iliyopita juni 11 mbele ya wanakijiji kubadilishana wake zao.Mr Wesonga akamchukua Ms Sara Mdua ambaye ni mke wa Woisi na Mr Woisi akamchukua Ms Annette Namataka ambaye ni mke wa Wesonga.Bwana Wesonga amezaa watoto watano na mke wake huyo wa zamani wakati Woisi amezaa watoto wawili na mke wake huyo wa zamani.

Category: HABARI | Views: 314 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-13 | Comments (0)




Mawakili wengi wa China wamenyanyaswa,kukamatwa na hata kufungwa jela lakini picha ya mmoja wao aliyekuwa na nguo zake zilizovuliwa na maafisa wa polisi imevutia hisia nyingi nchini China.
Category: HABARI | Views: 260 | Added by: nurdidy | Date: 2016-06-12 | Comments (0)